Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 25, 2018

Elimu juu ya Tetenasi (Tetanus)

Picha
Tetenasi  ni ugonjwa unaosababishwa na bacteria wanaoitwa ( Clostridium tetani). Wadudu hawa wanapatikana katika mazingira yanayotuzunguka mfano; ardhi, misumari au vitu vyenye ncha, vinyesi vya baadhi ya wanyama nk. Bacteria wa tetenasi wanaweza kuishi katika mazingira kwa miaka mingi. Pia wanapenda vidonda, ndio maana wanaingia mwilini kupitia vidonda au mikwaruzo. Dalili za Tetenasi zinatokea siku 4-14 baada ya kupata jeraha. Tetenasi imegawanyika sehemu mbili. Tetenasi inayotokea kwa watu wazima (adult) Tetenasi ya watoto (neonates)    Nani yupo hatarini kupata tetenasi? Kwa watu wazima (Adults)  Ikiwa umeumia na kupata jeraha  au kidonda sehemu ya mwili wako uko katika hatari ya kupata ugonjwa huu hatari wa tetenasi.  Ikiwa umetobolewa na msumari una zaidi ya 32% kupata tetenasi. Ikiwa umeungua, au watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya, au watu wanaojiwekea tattoo, watu wenye magonjwa ya meno, wapo katika hatari ya kupata ugonjwa...

Fahamu Madhara Ya Mirungi Kiafya

Picha
HISTORIA;  Ni mmea ambao una majina mengi kulingana na eneo,mfano gomba,miraa,mirungi nk. Shirika la afya duniani WHO limetangaza kuwa zaidi ya masaa 14.6 milioni yanapotezwa kila siku kwa ulaji wa mirungi huko Yemen. Ulaji wa mirungi ulianzia Ethiopia,ukaenea hadi nchi za Afrika Mashariki,Yemen, Zimbabwe, Zambia, Malawi na hata Afrika kusini. Mirungi ilionekana kuwa ni moja ya madawa ya kulevya hivyo ikakatangazwa na umoja wa mataifa UN na kupigwa marufuku mwaka 1971 kwasababu ya ufanano wa kemikali iitwayo amphetamine. Yapo madhara mengi ya kiuchumi, kidini nk. Lakini yafuatayo ni madhara ya kiafya ya mirungi kama ilivyofanyiwa utafiti na shirika la afya duniani; MADHARA YA KIAFYA;  *Mtumiaji wa mirungi yupo katika hatari ya kupata vidonda vya tumbo.  *Kupungukiwa msukumo wa kufanya tendo la ndoa (low sex drive) na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu.    *Ukosefu wa haja kubwa (constipation) *Utumiaji ...